Utapata nini katika tovuti hii?
Tovuti hii imeundwa nami N Kyalo. Na sina kitu kimoja cha kipekee ningependa kufanya na tovuti hii ila
kuitumia
kama pahala pangu pa kipekee kwenye mtandao.
Nitaongeza mengi hapa muda ukisonga na nina matumai ya
kwamba
nitaweza kupenda kazi nitakayoifanya hapa.
Kwa sasa, furahia sanaa yangu, maoni yangu ya vitabu mbalimbali na maandishi yangu.
Maoni ya vitabu nilivyovisoma
Nilipenda hadithi kutoka niwe mchanga. Nilionelea heri kusoma riwaya kuliko vitabu vya mtaala/silabasi
nilipokuwa shule ya upili.
Hii ni kwa sababu maisha shuleni ilikuwa ya kuhuzunisha kwani nilikuwa katika shule ya bweni.
Na basi nilitaka kuhisi ni kama nina uhusiano na maisha ya nje. Simu zilikuwa haramu shuleni na hata
kama
hazingeuwa, bado singekuwa nayo kwani babangu hangeninunulia.
Na hapa ndipo nilipoanza kupenda riwaya. zilikuwa zanisaidia kupunguza wwazimu wa kufungiwa shuleni
miezi
bin miezi.
Mapenzi yangu ya riwaya yalipotea kiasi nilipomaliza shule ya upili. Kwani sikuhitaji maburudisho
ya riwaya
tena. Nilikuwa na mtandao.
Nayo mtandao wenyewe ukawa wa kuhuzunisha kwani nimeyaona mengi na hakuna kinachonipendeza tena.
Ndivyo nikaja nikapatana na "booktube". Na nikapenda jinsi watu walipata furaha kwa usomaji wa vitabu.
Nmai nikaamua ni muda wangu wa kurudi kwa penzi langu la kale, fasihi.
Hapa utapata jedwali ya vitabu nilivosoma na
miezi na
miaka nilivyovisoma.
Utagubdua ya kwamba nimeweza kusoma kitabu kimoja tu kila mwezi... Ninag'ang'ana niwezavyo...😔
Fuata viungo kwenye jina ya vitabu hivyo na utaweza kujua maoni yangu ya vitabu hivyo.
Maandishi yangu
Nina nia ya kuandika pia. Si kusoma pekee. Lakini ninahadithi moja tu ambayo ningependa kuandika kitambo
niiage
dunia, Kyalo.
Basi nimekuwa nikijiambia ya kwamba sihitaji kubuni hadithi nyinginezo kwani hata mimi mwenyewe
ninaogopa
eti sitazipenda.
Ni jana tu, mnamo 16 wa Oktoba, 2025, nilipoamua hakuna haja ya kuogopa kuandika hadithi nyinginezo
zisizokuwa Kyalo.
Hadithi hizi zinaweza kunisaidia mimi mwenyewe niwe msimuliaji bora zaidi.
Nitazichapisha hapa mikipata nafasi na nguvu.
Na tafadhali, usiziibe... Tafadhali!!!