Uhakiki wangu wa The Will of The Many - James Islington.

Nina tabu kuita hii hakiki kwani ninawasilisha maoni yangu tu kuhusu kutabu chenyewe.
Nimefurahi sana kwani nimeweza kukimaliza kitabu changu cha kwanza kwa muda mrefu sana, miaka hata. Na nimeweza kukimaliza kitabu hiki kwa mwezi mmoja. Nilivutiwa na kitabu hiki. Mimi si shabiki wa ufalme wa Kirumi au kitu chochote cha Kirumi.
Ndio maana nilishangaa nilipopata ya kwamba nilikuwa nafurahia kitabu hiki. Kitabu chenyewe kiliniteka kwa mafumbo yake ambayo kwa bahati mbaya, hayakutatuliwa mwanzo kitabu kiliisha. Bado nina maswali mengi. Nilikuwa na tatizo la kutazama akilini kile nilikuwa nikisoma.
Hii nimepata ni shida yangu na si ya kitabu kwani nilisoma uhakiki wa mtu mwingine aliyependa jinsi mwandishi aliandika. Wengi wamesifia nathari ya mwandishi ni nimeachwa nikiponda shida yangu ni ipi.
Labda ni kwa sababu imekuwa muda mrefu tangu nikishike kitabu, labda ni kwa sababu sikujua ya kwamba nina tatizo la kutazama akilini nisomacho, sijui.
Ninaweza sema ya kwamba mhusika mkuu amezidiwa nguvu kwani hakuna kilichomshinda. Kila mara alikuwa na vidonda. Sidhani hiyo ni shida, lakini hiyo ni kuonyesha maisha yake yangekuwa yameisha mara kadha katika hadithi hili. Hakuna asichojua.
ambapo itabidi asaidiwe, lazima jambo litokee ndiposa aweze kuonyesha nguvu zake, akili zake, au vyote viwili. Yeye sio mdhaifu kwa chochote. Hakuna jambo mpya kwake.
Vikwazo vyake vilitokea kwa wengine. Si yeye. Alisemekana kua na shida za hasira kitabu kilipoanza. Lakini halikuwa tatizo tena alipojua hasira haitamsaidia. Na sisemi ya kwamba ningependa kumwona akiwa na hasira kila mara. La hasha!
Yeye kuwa wa asili ya kifalme na kuwa alifunzwa mengi utotoni inahisi kama njia ya urahisi kwa upande wa mwandishi. Sikumchukia mhusika mkuu huyu. Lakini sikumpenda pia. Sidhani ninaweza penda mhusika kama yeye. Nilipenda kitabu hiki licha ya yote niliyoyasema.
Ninajua chuki ya ushoga upo kwenye kitabu hiki lakini ningependa Eidhin asemekane kuwa shoga siku zijazo. Nimempenda mhusika huyu mno ingawa alisema machache zaidi kitabu mzima.