Uhakiki wa The yacoubian building - Alaa Al Aswany.

Kilichotasfiriwa na Humphrey Davis.
Onyo... unyanyasaji wa kingono kwa watoto, misimamo mikali ya kidini ya Kiislamu, mateso ya kingono, ubaguzi wa rangi....
Niliamua kusoma kitabu hiki baada ya kutizama video ambayo ilikuwa inazungumzia vitabu vya Kiafrica vilivyozungumzia haiba ya ujinsia moja. Na basi nilivutiwa zaidi baada ya kugundua kwamba kitabu hiki kiliandikwa na mwandishi kutoka Misri. Nilitaka kujua mfumo wa mawazo ya mhusika yeyote shoga katika kitabu hiki. Shoga huyu ni Hatim Rasheed. Naye, ni miongoni wa wahusika wakuu lakini si wa maana vile. Kama mwandishi angeamus kumtoa kwenye kitabu, tofauti ingekuwa ni ukubwa wa kitabu tu. Hii si kusema ya kwamba sioni umuhumu wake. La hasha! Misuko ya wahusika wengine wengi wakuu haikutani kamwe. Lakini ningependa vinginevyo. Hadithi yake Hatim si ya kupendeza. Mara si kunyanyaswa kingono akiwa mtoto (Na hapa ndipo nilidhani ya kwamba mwandishi alikuwa mwenye maono eti ushoga ni matokeo ya unyanyasaji wa ngono kwa watoto. Haikuwa ngumu kufikiria hivi kwani Hatim ndiye shoga pekee tunayefuata ambaye anataka mahusiano na wanaume wengine. Ninashuku Abd Rabbuh si shoga. Yeye ni malaya tu kwa Hatim. Lakini nilibadilisha maono yangu kwa sababu mwandishi aliandika ngono kati ya Hatim na Abd kwa urembo. Urembo ambao haungekuwepo kama mwandishi alifikiria ushoga kama zinaa.), mara si mapenzi na mtu ambaye hamtaki. Mara anaishi maisha yake akimtafuta yeyote anayefanana na yule mfanyakazi ambaye alimnyanyasa akiwa bado mchanga. Kusoma hadithi yake ilikuwa ngumu kwani ilikuwa rahisi kutabiri kitakachomtokea. Lakini Hatim alikuwa kipofu mkubwa sana. Nilimpenda Zaki Bey japo si sana. Kwani alijiona bila laumu ila alimdhulumu mfanyikazi wake Abaskharon. Japo hakumtendea mabaya mno, nilisumbuka kila mara hakuona makosa yake kwani alidhani hivyo ndivyo wafanyakazi hushughulikiwa. Silalamiki eti aliweza kupata mwisho mwema, la hasha, kwani nilipenda ambavyo hadithi ya Busayna iliweza kuisha. Busayna ndiye mhusika nimpendaye zaidi kwa kitabu hiki. Na nina furaha kwa sababu aliweza kupata alichotaka. Naye Taha el Shazli, niseme nini jameni? Kwa kuwa mwanafunzi mwerevu, alikuwa mwanaume mpumbavu sana. Huyu ni mwengine niliona mwisho wake kutoka mbali. Na ni mwisho ambao niliweza kuufurahia ingawa ninasumbuka nikifikiri anafikiria vivyo hivyo.h!! Souad Gaber!!! Mhuski wa kusikitisha mno katika kitabu hiki. Mwanamke mwenye ujasiri na hodari. Sikupenda mwisho wa hadithi yake hata kidogo. Ningependa mwisho wake uandikwe upwa kama hiyo ni haki niliyokuwa nayo. Cha kusikitisha zaidi ni ya kwamba sikuridhika na mwisho wa hadithi yake Hagg Muhammad Azzam hata kidogo. Ndiyo, alidharauliwa kitabu kilipokuja kuisha, ndiyo, alihisi vibaya. Lakini hiyo hailingani na robo ya yale Souad aliyoyapitia kwa sababu yake. Hiki ni kitabu kilochojaa kinaya. Mara si waumini kuwa wafisadi, mfano Hagg 👀. Nilipenda kitabu hiki. Kilinionyesha mengi sikuyajua kuhusu Misri na wananchi wake. Na kilinionyesha maisha ya wanamisri kadhaa na jinsi ufisadi serikalini inavyowaathiri. Niliweza kuona jinsi uhusika wa Misri na nchi mbali mbali ilivyo. Niliona ndoto za wanamisri na jinsi jamii ya kimisri huwa. Hiki ni kitabu kilichonionyesha mengi na ninafuraha nilikisoma. Sentensi zake ni refu kuliko kiasi na bado ninawaza kama hivyo ndivyo sentensi za Kiarabu huwa...